0



Kampeni  za  uchaguzi  mdogo  wa  ubunge  katika  jimbo  la  Kalenga, Iringa  vijijini  zimeanza  kuchukua  sura  mpya  baada  ya  chama  cha  demokrasia  na  maendeleo  (  CHADEMA )   kuanza  kutumia  helikopta  ambapo  kwa  siku  watafanya  mikutano  sita.....

Mwenyekiti  wa  chama  hicho  taifa, Bw. Freeman  Mbowe, alisema  chama  hicho  kitapasua  anga  ya  jimbo  hilo  kupitia  kauli  mbiu  yao    ya  "Anga  kwa  anga, Kofia  na  kanga  sasa  basi", akiongoza  mashambulizi  hayo  ili  kumpigia  kampeni  mgombea  wao, Bi  Grace  Tendega....

Alisema   helikopta  hiyo  itapita  mtaa  kwa  mtaa, kata  kwa  kata, kijiji  kwa  kijiji, tarafa  kwa  tarafa.

Katika  hatua  nyingine, wakazi  wa  jimbo  hilo  wametahadharishwa  kutoikimbilia  helikopta  ya  CHADEMA  kwa  kuwa  ina  athari  kiafya....

Katibu  wa  CCM  mkoani  Iringa, bw. Hassan  Mtenga  aliyaema  hayo  juzi  wakati  akimnadi  mgombea  wa  CCM, bwa. Godfrey  Mgimwa  katika  mkutano  wa  hadhara  uliofanyika  kwenye  kata  ya  Luhota, jimboni  humo....

"Tunasikia  CHADEMA  wanataka  kuleta  helikopta  ili  kukusanya  watu  kwenye  mikutano  yao  baada  ya  kuona  wananchi  hawafiki  kwenye  mikutano  yao.Naomba  nitoea  tahadhari, mkiiona  msiende  kwani  helikopta  zina  madhara  kiafya", alisema  bwa. Mtenga

Alisisiza  kuwa  moshi  unaotoka  katika  injini  ya  helikopta  una  madhara  kiafya  na  mara  nyingi  husababisha  kansa, hivyo  hakuna  sababu  ya  kusogelea  karibu...

Alisema  athari  za  kuisogelea  helikopta  zinaweza  zisijitokeze  sasa  lakini  baada  ya  muda  fulani, zitaanza  kujitokeza, hivyo  aliwataka  wakazi  wa  jimbo  hilo  kuwa  makini....

"Ushauri  wangu, wakija  na  helikopta  zao  msiende, endeleeni  na  kazi  zenu  maana  mkivuta   moshi  wa  helikopta  mtaathirika", alisema  na  kuongeza  kuwa  CCM  inauhakika  wa  kushinda  katika  uchaguzi  huo.....

Kwa  upande  wake  bwana  Mgimwa  amewahakikishia  wakazi  wa  jimbo  hilo  kuwa  kama  watampa  ridhaa  ya  kuwa  mbunge  wao  atamaliza  tatizo  la  maji  ambalo  limedumu  muda  mrefu  katika  kijiji  cha  Kibena, kata  ya  Ifunda....

Alisema  mbali  ya  changamoto  nyingi  zilizopo  kijijini  hapo,tatizo  la  maji  ndio  limeonekana  kuwa  sugu  hivyo  atakwenda  kuzungumza  na  waziri  wa  maji, Profesa  Jumanne  Maghembe  ili  amweleze  hitaji  la  maji  kwa  wanakibena...

"Ndugu  zangu  natambua  kuwa  kijiji  hiki  kinatatizo  kubwa  la  maji, hivyo  kama  mtanipigia  kura  za  kutosha  na  kuwa  mbunge  wenu  ntahakikisha  nalimaliza", alisema.

Wakati  huo  huo,mwenyekiti  wa  CHADEMA  kijiji  cha  Wangama, bw. Fred John, ametangaza  kukihama  chama  hicho  na  kujiunga  CCM. Kijiji  hicho  ndicho  alichozaliwa  mgombea  ubunge  wa  jimbo  hilo  kwa  tiketi  ya  CHADEMA,Bi Tendega...

Akizungumza  mbele  ya  viongozi  wa  CCM   na  wakazi  wa  eneo  hilo, bw. John  alisema  ameamua  kuhama  CHADEMA  kwa  hiari  yake  kwani  alikuwa  anapotea....

"Niwahakikishieni  wakazi  wa  kijiji  hiki, nitarudisha  wote  waliokuwa  CHADEMA  kwani  mimi  ndiye  niliyefanya  kazi  ya  kuwahamasisha,sasa  mwamba  umevunjika",  alisema

Awali,  katibu  wa  CCM  mkoani  Mtwara, Shaibu  Akwilombe  aliwaambia  wakazi  wa  kijiji  hicho  kuwa  bi. Tendega  hana  ilani  ya  uchaguzi  wala  serikali  hivyo  hawezi  kuleta  maendeleo....

Alisema  kuwa  ili  maendeleo  yapatikane  Kalenga, wananchi  wanapaswa  kumchagua  mgombea  wa  CCM, Bw. Mgimwa.

"Grace  ni  dada  yetu,ndugu  yetu, rafiki  yetu  na  jamaa  yetu, lakini  tusimpe  nafasi  ya  kuwa  mbunge  kwa  sababu  CHADEMA  hakina  Ilani  wala  serikali....Mpeni  kura  zote  Mgimwa  ili  aweze  kuwaletea  maendeleo", alisema  Akwilombe

Post a Comment

 
Top