Watu wa karibu wa Mtuhumiwa huyu walijitokeza Mahakamani ili kuangalia kama ndugu yao aitwae Simon Ngozi (21) ataweza kupata dhamana kwenye kesi inayomkabili ya kubaka mtoto wa miaka tisa.
Mshukiwa huyu alikuwa kortini kujibu tuhuma za kumbaka mtoto wa miaka
tisa April 2014 ambapo wakati anataka kumbaka Mwanamke huyu Mahakamani
tena kwenye eneo la wazi, alimpiga mtama kwanza Mwanamke huyo lakini
kwenye purukushani zake hakufanikiwa manake Polisi walimuwahi.
Shughuli za Mahakama zilisimama kwa muda baada ya tukio hilo kutokea
ambapo baada ya hapo Mwanamke aliyetaka kubakwa alisema, "Nilikua nimeketi
karibu naye na mara ya kwanza alilishika begi langu nikalisogeza mbali
nikidhani ni mwizi lakini bila aibu akanishikashika tumboni kabla ya
kunisukuma nikaanguka sakafuni"
Baada ya hapo dada wa mtuhumiwa alimuomba mwanamke huyo kumsamehe
ndugu yake akisema yuko katika hali hiyo baada ya mchumba wake kumtoroka
kwa sababu ya kesi ya ubakaji.
Post a Comment