MKONGWE wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amedaiwa kubatizwa juzikati
katika Kanisa Katoliki Nyalikungu wilayani Maswa, Simiyu lakini mwenyewe
amekanusha.
Chanzo makini kilichodai kushuhudia ubatizo, kilieleza kuwa Johari alifika Jumapili kanisani hapo na watu kuhoji kwa nini achelewe kubatizwa? Alipotafutwa na mwanahabari wetu, Johari alitiririka:
“Kweli nilikwenda kwenye hilo kanisa lakini sikubatizwa kama alivyosema huyo mtu. Nitabatizwaje mara mbili? Mimi nilishabatizwa tangu utotoni.”

Post a Comment