0
Huwa si kitu cha ajabu kuona mapacha wakifanana kila kitu ndani ya familia hadi kusababisha watu kuwachanganya pindi wanapokutana nao kama hawajawazoea kuwaona kila siku.
Na mara nyingi mapacha wamekua wakishirikiana katika vitu mbalimbali lakini haijawahi kufikia hatua ya kushirikia hadi mambo ya ndani kabisa kama vile akaunti,mishahara na hatamahusiano na mwanaume mmoja eti kwa vile tu ni mapacha,,Hii inashangaza kidogo.

twinooo
Huko nchini Australia mapacha waliozaliwa kwa kupishana dakika moja Anna na Lucy Decingue wenye miaka28 wanashirikiana kila kitu maishani gari,akaunti ya facebook,benki,mshahara,kazi hata kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mmoja yote huyafanya kwa kushirikiana.
Katika Makala iliyotolewa na Gazeti la MWANANCHI limeeleza kuwa Mabinti hao pia wanatumia kiasi kikubwa cha fedha kufanya upasuaji wa kuondoa kitu chochote kinachowafanya wasifanane na tayari wamefanya usapuaji wa kuongeza matiti katika kiwango kimoja ili ufanano wao upaki kama ulivyo,pia wametengeneza midomo,kope na mambo mengine mengi ya kulinda ufanano wao.
makeup 
Matumizi yao ya kukarabati mwili yamewagharimu kiasi cha dola za kimarekani zaidi ya laki mbili sawa na milioni 365.6 na ni nadra sana kuwakuta hawapo pamoja na mpaka sasa bado wanaishi na mama yao mzazi licha ya kuwa na umri wa kuolewa.
Wanasema kwa sasa wana uhusiano na mwanaume mmoja tu ambaye kazi yake ni fundi umeme na kila mmoja ameridhika na hana kinyongo,ubaguzi wala chuki na mwenzake na ikifika wakati wakimchoka hushirikiana jinsi ya kumpata mwingine.
“Tuna rafiki mmoja wa kiume na tunalala nae kitanda kimoja,tuna ladha na hamu zinazofanana kwa kila mtu,tunashirikiana kwenye mapenzi pamoja, chumba kimoja na tumekua tukifurahia maisha yetu na kama ikitokea tukashindwa tabia za rafiki yetu wa kiume tunatoa uamuzi wa pamoja kutafuta mwingine “Anasema Lucy.
Pamoja na kushirikiana kila kitu pia wanafanyakazi moja na cheo walichopewa ni kimoja hivyo wanalipwa mshahara mmoja na si miwili.

Post a Comment

 
Top