0
Staa wa Nigeria David Adedeji Adeleke maarufu kwa jina la Davido, ameamua kuchota sehemu ndogo ya pesa nyingi alizofanikiwa kuingiza mwaka huu, na kuwanunulia zawadi za magari ya kifahari watu wake wawili muhimu ambao wana mchango mkubwa katika mafanikio ya kazi zake za muziki anayoendelea kuyapata.

Davido amemzawadia meneja wake Kamal Ajiboye gari aina ya Mercedes 450 GL pamoja na producer wake aitwaye Shizzi amempa Porsch Cayenne.

davido zawadi
Kupitia Instagram yake Davido ameshare picha ya magari hayo (hapo juu) na kuandika:
“CONGRATS MY MANAGER @KAMALAJIBOYEAND MY ACE PRODUCER @iamshizzi issue!! my whole team dey chop!”.

Post a Comment

 
Top