0
Waziri wa nchi anayehusika na Maadili nchini Uganda, Simon Lokodo amelitaka jeshi la polisi kumhoji mwanamuziki Desire Luzinda kutokana na picha zake za utupu zinazodaiwa kupigwa na rafiki yake wa kiume ambaye ni MNigeria.

Akiongea na gazeti moja la nchini humo waziri Lukodo amesema tayari ameliagiza jeshi la polisi kuwakamata wahusika na kwa sasa jeshi hilo lipo mbioni kumkamata Luzinda na rafiki yake huyo wa kiume.
 

Waziri huyo amesema Luzinda na rafiki yake huyo wa kiume watashitakiwa kwa kuonyesha picha za utupu, chini ya kifungu namba 13, cha Sheria ya kukabiliana na picha za ngono.

Post a Comment

 
Top