Watu 15 wamejeruhiwa kutokana na mlipuko
wa bomu katika baa maarufu ya Arusha Night Park katika eneo la Mianzini
katika jiji la Arusha.
Tukio hilo lilitokea jana saa mbili usiku wakati
mamia ya watu wakiwa katika baa hiyo wakiangalia mechi ya soka ya Ligi
Kuu ya England kati ya Chelsea na Swansea. Chelsea ilishinda 1-0.
Mmoja wa wamiliki wa baa hiyo, Angelo Mwoleka pia alithibitisha kutokea mlipuko huo na kueleza kujeruhiwa watu kadhaa.
“Ni kweli kuna mlipuko umetoka na watu kujeruhiwa, mimi sikuwepo ila nipo njiani nakwenda eneo la tukio, “alisema.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, John Lymo
alisema watu saba waliumia vibaya kutokana na bomu hilo na walipelekwa
katika Hospitali ya Mkoa Arusha ya Mount Meru.
Akizungumzia tukio hilo, Mkuu wa mkoa wa Arusha, mh. Magesa Mulongo, ambae ni kiongozi wa Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa amesema watu 15 wamejeruhiwa kwenye mlipuko huo.
Amesema
majeruhi wote wamepelekwa hospitali ambapo uchunguzi wa awali
umeonyesha kuwa bomu hilo ni la kutengenezwa kwa mkono na mpaka sasa
hajajulikana alietekeleza shambulio hilo.
Mulongo pia
amesema hakuna mtu aliyepoteza maisha kwenye shambulio hilo ambalo
uchunguzi wa awali umeshatoka, ila baadae itatoka taarifa rasmi pale
uchunguzi kamili utakapokamilika.
Tukio hilo limekuja wakati bado jiji la Arusha
likiwa na kumbukumbu ya kushambuliwa kwa mabomu kwa Kanisa la Mtakatifu
Joseph Mfanyakazi lililopo eneo la Olasiti na jingine Uwanja wa Soweto
wakati Chadema walipokuwa wakifunga kampeni za uchaguzi mdogo wa
udiwani.
Katika matukio yote hayo, watu sita waliuawa na wengi kujeruhiwa.
Katika matukio yote hayo, watu sita waliuawa na wengi kujeruhiwa.
Post a Comment