0

 

Rapper Shetta alipata ajali mbaya ya gari wakati akielekea Babati, mkoani Manyara kufanya show, lakini Mungu alimnusuru yeye na watu wengine wawili aliokuwa nao katika gari hilo.
 
Akiongea na  Times 100.5  Fm, rapper huyo amesimulia jinsi ajali hiyo ilivyotokea ambapo ametaja chanzo cha ajali hiyo ni kumkwepa pundamilia aliyekuwa akikatiza barabarani.
 
“Mi nilikuwa natoka Dar na ndege mpaka Arusha, mimi nilikuwa na show Babati jana. Arusha mpaka Babati ni masaa mawili au matatu. Kufika njiani kuna sehemu inaitwa Minjingo kama sikosei kuna wanyama wanyama hapo. Tulikuta pundamilia mmoja barabarani, alikuwa ameshavuka…sasa wakati gari pia haijavuka nae alikuwa anataka kurudi tena huko halafu gari ilikuwa speed kidogo, sasa katika kupigapiga break ndio gari ikapinduka.” Ameeleza Shetta.
 
“Gari imeumia sana lakini sisi hatukuumia hiivyo, ni maumivu tu ya kawaida. Hapa nilipo ndio naelekea hospitali kufanya checkup ya mwili kama kutakuwa na internal effects lakini kwa nje niko vizuri sana.” Ameongeza Shetta.
 
Ameeleza kuwa ilibidi show yake iahirishwe hadi jana  jumamosi  kwa kuwa kila mtu alikuwa amepata taarifa kuhusu ajali hiyo.
 
Katika hatua nyingine, rapper huyo ameeleza kuwa alikuwepo mtu aliyepokea pesa ya show hiyo kwa jina lake hivyo baada ya waandaaji kwenda Dar walifanikiwa kupata namba halisi ya Shetta ambaye walimuomba awasaidie kufanya show hiyo ili kulinda jina lao kuliko kuahirisha.
 
Hata hivyo, Shetta amesema tayari polisi wanamshikilia mtu aliyekuwa amewaunganisha waandaaji hao na Shetta feki na kwamba anatamani kuongea nae ili afahamu undani wa mchezo huo wa kitapeli.
  
Source: Times 100.5 fm

Post a Comment

 
Top