0
collage
Baada ya diamond kuachia nyimbo yake  ya Mdogomdogo mapema wiki hii, hit single iliyopokelewa vizuri sana na watanzania wengi, huku kila mmoja akiwa anasubiria kwa hamu jinsi video ya wimbo huo utakavyokuwa, kwa mujibu wa Diamond Platnumz mwenyewe anasema, wimbo huo ni kwa ajili ya wa tzee kwanza, ila homa ya jiji na ya bara zima la africa inakuja mapema wiki ijayo.
Diamond & Iyanya
Diamond Platnumz ameanza kuwa na utaratibu mpya unaomfanya atoe nyimbo mbili kwa pamoja, ya kwanza ikiwa kwa ajili ya watzee, na kama fans wa nchi nyingine hawataielewa, basi kuna nyingine inayotoka hivi karibuni kwa ajili ya bara zima, hii ni kutokana na staili tofauti anazotumia kuwakosha nyoyo mashabiki wake wa kila pande za dunia. Sauti ya Iyanya ndio itakayosikika kwenye nyimbo yake mpya, Iyanya akiwa ni msanii anayekubalika huko West Africa zaidi hata ya Davido, hii inatarajiwa kumuweka Diamond Platnumz kwenye ukurasa mpya wa muziki.

Post a Comment

 
Top