MKONGWE
kwenye sanaa za Kibongo, Blandina Chegula ‘Johari’ amesema kufuatia
vifo vya mfululizo vya wasanii, kwa kiasi kikubwa wasanii wamebadilika
kitabia.
Akipiga stori na paparazi wetu alisema, wasanii hao wamejitambua kuwa
duniani watu wanapita, jambo ambalo kwa muda mrefu walikuwa wamelisahau
na kuponda raha mfululizo.
“Tangu wenzetu wafariki mfululizo, wasanii wengi tumepata mshtuko na kujitambua, naona wengi wamebadilika, wamenyooka na kuanza kumrudia Mungu,” alisema Johari.
Vifo vya wasanii vilivyotokea hivi karibuni ni pamoja na cha Adam Kuambina, Sheila Haule ‘Recho’ na George Tyson.
“Tangu wenzetu wafariki mfululizo, wasanii wengi tumepata mshtuko na kujitambua, naona wengi wamebadilika, wamenyooka na kuanza kumrudia Mungu,” alisema Johari.
Vifo vya wasanii vilivyotokea hivi karibuni ni pamoja na cha Adam Kuambina, Sheila Haule ‘Recho’ na George Tyson.
Post a Comment