Viti vikiwa vimetawanywa baada ya vurugu zilizosababishwa na mgomo huo.
WANAFUNZI wanaolipiwa na Bodi ya Mikopo katika Chuo cha Taifa cha
Usafirishaji (NIT) kilichopo Mabibo Mwisho jijini Dar, leo wamegoma na
kufanya vurugu wakidai kucheleweshewa fedha zao za mkopo. Mgomo huo
umeanza majira ya saa 6 na nusu mchana ambapo polisi waliingilia kati
kutuliza ghasia zilizokuwa zinaendelea chuoni hapo. Mpaka mtoa habari
hii anaondoka eneo la tukio, bado wanachuo walikuwa wakisubiri majibu ya
uongozi wa chuo hicho
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment