0

http://api.ning.com/files/pVOWqi0dq18zEVY-0VLQlEbTbHxSD3N84cADcr9ozulkbAyZWyAtbW-SLeJHHE*tdyxagHUYOdKvorWKNl8IALJcXo1qU*6u/1yanga1.JPG
Timu ya Yanga SC imeondolewa kwenye Michuano ya Klabu Bingwa Barani Afrika baada ya kufungwa na Al Ahly kwa penalti 4-3 katika mechi iliyochezwa Uwanja wa El Max Haras El Hodod jijini Alexandria, Misri!
Mpaka dakika ya 90 ya mchezo, matokeo ya jumla yalikuwa 1-1 hivyo kuamriwa kupigwa mikwaju ya penalti ambapo Yanga walipata 3, wakati Al Ahly wakipata 4.
Wachezaji wa Yanga waliofunga penalti ni Didier Kavumbagu, Emmanuel Okwi na Nadir Haroub 'Cannavaro' wakati Oscar Joshua, Mbuyu Twite na Said Bahanuzi wakikosa mikwaju hiyo.
Kwa matokeo hayo, timu ya Al Ahly imefuzu katika hatua ya 16 bora ya michuano hiyo

Post a Comment

 
Top