0

mafikimond-2

Kulikuwa na rumors hapo mwanzo kuwa Diamond yupo studio akipika moja ya colabo matata sana huko nchini sauzi pamoja na kundi la mafikizolo, na hata baadhi ya picha ali-post akiwa anaonekana yuko studio na kundi hilo la muziki, umbea huo umesibitishwa tena kuwa na ukweli wa asilimia mia moja na mmoja wa Dj maarufu hapo south, ambaye ndiye anayesemekana anasimamia swala zima la nyimbo hiyo, jamaa maarufu sana, anajulikana kama Oskido, kupitia account yake ya instagram alifunguka kuwa yupo studio akitengeneza ngoma hiyo.

Oskido-The-7th-Commandment
Oskido ambaye ni mzimbabwe anayefanyia kazi zake za u-DJ afrika ya kusini, alishawahi anatajwa kuwa ndiye nguli wa kutengeneza kwaito huko bondeni, aliwahi pia kutajwa kama one of the Top 10 kwaito legends of all time by DStv’s MTV Base. anasifika kutengeneza nyimbo kali zinazo-make headlines hivi sasa, na kusifika zaidi kwenye umahiri wake mkubwa wa kutengeneza vionjo vya nyimbo ya kuchezeka hivyo kuipa ladha flani hivi nyimbo, Oskido anafananishwa na David Gueta wa marrekani kwa umahiri wake katika kupaisha nyimbo na kuifanya ikubalike hata kwa mtu ambaye hailewi lugha inayotumika kwenye wimbo.Hii ni moja ya kazi ya Oskido inayo make headlines hivi sasa, akimshirikisha May D.

Post a Comment

 
Top