Home
»
WASANII
» Mapenzi ya Justin Bieber na Selena Gomez sintofahamu!!
Kukiwa bado kuna hali ya sintofahamu kati ya mapenzi ya
Justin Bieber na Selena Gomez, hivi karibuni Justin alifanya kitendo
ambacho kinazidi kuwaweka watu njia panda juu ya mahusiano yao. Hii
ilitokea baada ya Justin Bieber kupost picha kwenye mtandao wa Instagram
ya yeye akiwa amekumbatiwa kichwa na ex wake Selena huku kukiwa na
caption isemayo “ur love is unconditional”, hii ilikuwa Jumatano ya
tarehe 11/06/2014. Lakini cha kushangaza, post hiyo haikudumu, Justin
alii delete muda mfupi tu baada ya kui post na kuacha watu wakiwa na
maswali kibao, je alikuwa anamaanisha alichoki post? Kwanini amei
delete? Ni maswali ambayo majibu yake nadhani watakuwa nayo wawili hao.
![all-justin-bieber-photos-113](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_v_oqrkc8_XpHIvGt-QFJXwn85MkQUMqH0NmyEOjLfQ8ArfoI-D74Avj-LzkP3PARK4LYgvtY0q4Pylzh9p-A_9zvG248sAPayhrfzlh4ynJjD1y_WTt-fG7f-PtaHRFcBvpIJpQzG2CVjZfaALZyg=s0-d)
Hivi karibuni Bieber na Selena hawako kwenye good terms kuanzia kipindi
flani hivi cha April, na hawajaonekana pamoja toka kipindi hicho.Kama
kutakuwa na update yeyote ile, basi usitie shaka, Vibe Magazine Tz tupo
kwaajili ya kuwajuza, hakikisha tu unatembelea website yetu
(www.vibe.co.tz) na app mara kwa mara kupata habari motomoto na za
uhakika.
Post a Comment