Juzi, Nuhu Mziwanda alipost picha kwenye Instagram ikionesha Tattoo aliyochora yenye jina la mpenzi wake Shilole ikiwa imeandikwa ‘ShiShiBaby’.
Wengi walihoji kuhusu tattoo hiyo kuwa ni tattoo inayodumu au ni ya kuonesha kwa muda itafutika.
Katika Majibu yake, Mziwanda alieleza kuwa tattoo aliyochora ni ya kudumu katika kipindi
chote atakachokuwa duniani na kwamba haitafutika mpaka siku anaingia
kaburini.
Je,
itakuwaje wakiachana (hatuombei iwe hivyo)? Nuh ameeleza kuwa yeye
hajali kama wataachana au vipi kwa kuwa Shilole ni mtu muhimu sana kwake
na amefanya kwa mapenzi yake.
“Nilimwambia labda wewe ndio utakaekuja kunizingua lakini mimi hata
siku moja sitakuzingua. Hata kama tukiachana, mimi nimeamua hivyo na
nimefanya kwa mapenzi yangu kwa sababu nampenda sana na ni mtu muhimu
sana kwangu.”


Post a Comment