0
Aunt Ezekiel.
BAADA ya wiki iliyopita kumaliza mahojiano na Miss Tanzania 2006 aliye pia mwigizaji wa sinema za Bongo, Wema Isaac Sepetu, wiki hii tunaye supastaa mwingine.
Anaitwa Aunt Ezekiel Grayson, si jina geni kwa wadau mbalimbali wa burudani nchini. Ni mrembo ambaye amepata jina kubwa kupitia sanaa yake ya uigizaji wa filamu aliyoianza miaka saba iliyopita.
Msanii huyo ambaye ni mtoto wa damu wa aliyekuwa mchezaji mahiri wa Simba Sports Club ‘Wekundu wa Msimbazi’ marehemu  Ezekiel Grayson.
Aunt Ezekiel amepitia maisha  magumu sana kabla
 ya kufika alipo leo. Ili kujua maisha yake halisi ungana na mimi, Imelda Mtema.
Mwandishi:  Mambo Aunt? Natumaini uko mzima. Mimi ningependa kujua zaidi historia ya maisha yako kuanzia ulikotokea hadi ulipo sasa.
Aunt: Duu! Sawasawa! Mimi nimezaliwa  mwaka 1988 hapahapa jijini Dar es Salaam. Ni mtoto wa pili kwa mama yangu mzazi kwa sababu kwa  baba  nina ndugu zangu wengine.
Mwandishi: Kwa hiyo una maanisha kabla ya baba yako kuwa na mama yako alikuwa na mwanamke mwingine?
Aunt: Ndiyo.
Mwandishi: Wakati huo ulikuwa ukiishi hapa Dar es Salaam sehemu gani?
Aunt: Nilikuwa nikiishi Ilala  na nilipata elimu yangu ya msingi katika Shule ya Msingi Bunge mwaka 1995 mpaka 1998, nikaenda kumalizia Kisarawe, Pwani.

Post a Comment

:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

LAANA

 
Top