Mabingwa hao wa 2010 walipoteza mechi yao ya kwanza dhidi ya Uholanzi baada ya kulala kwa bao 5-1 kabla ya jana kupigwa tena na Chile.
Kwa matokeo ya jana, Hispania wanashikilia mkia katika kundi B wakiwa hawana pointi yoyote wakitofautiana mabao ya kufungwa na wenzao Australia ambao nao hawana pointi. Timu hizo zisizo na pointi zitakutana katika mechi yao ya mwisho Juni 23 mwaka huu.
Kundi hilo linaongozwa na Uholanzi wenye pointi 6 baada ya kushinda mechi zote mbili walizocheza.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.