Mbunge Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Samwel Nassari amefunga
ndoa na Anande Nko kwenye Kanisa la Pentekoste lililopo Kilinga, Arumeru
jijini Arusha ikifuatiwa na sherehe kubwa iliyofanyika katika Viwanja
vya Usa-River Academy jirani na Hoteli ya Ngurdoto.
Sherehe
hiyo ilianza mishale ya saa 7:00 mchana siku ya leo ambapo watu wote
walialikwa wakiwemo ndugu, marafiki, jamaa na wananchi wote wa Arumeru
Mashariki ambao wamepiga ‘mpunga’ wa kutosha na vinywaji hadi kila mtu
akaondoka akisema ‘Nassari ameacha historia’.
Post a Comment